エピソード

  • Hali ya siasa Afrika Mashariki na mizozo ya DRC na Sudan: Kulikoni Podcast
    2023/04/26
    Katika msururu wa leo wa kipindi cha Kulikoni, Prof Monda anaongea na Bwana Goodluck Paul, mwandishi wa masuala ya diplomasia anayefanya na runinga ya Azam kutoka Taifa la Tanzania. Wanaangazia siasa za Afrika mashariki na mizozo ya DRC na Sudan. Karibu!
    続きを読む 一部表示
    42 分
  • Nilikuwa darasa moja na Dr. Ruto, Rais Mteule
    2022/08/17
    Esther Cherobon alikuwa katika darasa moja na Rais Mteule, William Ruto katika Shule ya Msingi ya Kamagut kwenye Eneobunge la Turbo katika Kaunti ya Uasin Gishu. Cherobon anasema kuwa Ruto alikuwa mwerevu sana shuleni na alipofanya mtihani wa wa CPE mwaka 1980 aliibuka wa kwanza kwenye eneo zima kwa kupata alama 33 juu ya 36. Anasema wazazi wa Ruto walikuwa waanzilishi wa kanisa la AIC hivyo kumkuza pamoja na nduguze kwa kuzingatia dini. Licha ya kulelewa katika mazingira ya umasikini, Ruto alitia bidii masomoni akilenga kubadili hali yake na ya familia yake. Faith Kutere amemhoji kwenye Siasa Podcast wiki hii.
    続きを読む 一部表示
    23 分
  • Daily Brief Podcast; Is Uhuru learning from DP Ruto? Episode 1
    2022/06/20
    Was the chaos in Jacaranda a prelude to what could happen nationally after the August 9th polls? Who was to blame for the altercation that saw UDA aspirant, Francis Mureithi injured? In a separate incident, President Uhuru donates Sh10 million to the Akorino church and offers them a piece of land worth more than Sh100 million. Is this a case of trying to gain political mileage in church or is the head of state honouring the now 100-year old religious faction? We also dissect the remarks of Moses Kuria targeting DP Ruto and his UDA party and the viral video of Kabogo campaigning for Raila Odinga. Is this a case of betrayal in the mountain or are the Kiambu politicians just trying to get the attention of DP Ruto? Kimani Mbugua takes a look at all these and more on the Standard podcast.
    続きを読む 一部表示
    5 分
  • Uteuzi tata hadi mgombea huru; Timothy Toroitich
    2022/06/08
    Wakili Timothy Toroitich, mwaniaji wa kiti cha ubunge kwenye eneo la Marakwet Magharibi ni miongoni mwa wagombea huru wengi waliojitokeza Kaskazini mwa Bonde la Ufa baada ya kutoridhishwa na matokeo ya shughuli ya uteuzi wa Chama cha UDA. Faith Kutere amezungumza naye kuhusu safari yake ya siasa, idadi kubwa ya wagombea huru waliojitokeza nchini, ukosefu wa usalama kwenye Bonde la Kerio, mipango yake ya kisiasa iwapo atachaguliwa miongoni mwa masuala mengine.
    続きを読む 一部表示
    18 分
  • Siasa Podcast. Lonyangapuo: Kibaki alinikuza kisiasa
    2022/04/23
    Wiki hii katika Siasa Podcast tunaangazia maisha ya Hayati Mwai Kibaki ambaye alikuwa Rais wa tatu wa Taifa la Kenya. Kibaki anakumbukwa kuwa kiongozi aliyebuni mbinu mbalimbali za kuinua uchumi wa taifa na kukabili chagamoto zilizokumba taifa. Aidha, alizipa nafasi jamii ambazo zilihisi kutengwa wakati wake nafasi uongozini. Faith Kutere amezungumza na Gavana wa Kaunti ya Pokot Magharibi, John Lonyangapuo ambaye anadai kuwa safari yake ya kisiasa ilianza baada ya Mwai Kibaki kutambua jamii yake na kumpa nafasi ya kwanza ya uongozi akiwa Katibu Mkuu katika Wizara ya Viwanda.
    続きを読む 一部表示
    13 分
  • Siasa Podcast; Ahadi za Raila na Ruto; watatekeleza? Maoni ya Wakenya
    2021/10/16
    Wakenya wanatoa maoni kuhusu ahadi za Raila Odinga na William Ruto. Baadhi wanasema ahadi zao ni ndoto tu huku wengine wakiwa na matumaini kwamba watatekeleza. Aidha, Wakenya wameshabikia kuharamishwa kwa mpango wa Huduma Namba. Je, rufaa ya serikali itafaulu? Wanahabari wetu wameshiriki gumzo na Wakenya kuhusu masuala haya.
    続きを読む 一部表示
    20 分
  • Siasa Podcast: Hatutaki Siasa Makanisani - Askofu Anthony Muheria
    2021/09/13
    Hatua ya Kiongozi wa Kanisa la Kianglikana, Jackson Ole Sapit kuwanyima fursa wanasiasa kuhutubu katika mimbari kwenye halfa aliyokuwa akiongoza katika Eneo Bunge la Butere, Kaunti ya Kakamega, imeendelea kuibua mijadala mikali. Je, ndio mwisho wa maendeleo na ujenzi wa makanisa baada ya wanasiasa kunyimwa fursa ya kuzungumza mimbarini? Mwanahabari wetu Victor Mulama amemhoji Askofu wa Kanisa Katoliki Dayosisi ya Nyeri Anthony Muheria ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Madhehebu la Kushughulikia Kanuni za Kuzingatiwa katika Maeneo ya Ibada.​
    続きを読む 一部表示
    13 分
  • Siasa Podcast; Uhuru asimnyanyase Ruto, asema Didmus Barasa
    2021/08/27
    Mbunge wa Kimilili, Didmus Barasa anasema kuwa uhusiano mbaya kati ya Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake, William Ruto ni kutokana na siasa. Katika mahojiano na Faith Kutere, Barasa anasema hatua ya Rais kumwambia Naibu wake ajiuzulu haifai. Aidha, amepuuza uwezekano wa Ruto kuondolewa kupitia hoja ya kutokuwa na imani naye bungeni.
    続きを読む 一部表示
    12 分